Msaada katika mahakama

Help at court - Swahili (Kiswahili)

Kuna njia nyingi za kupata msaada katika mahakama. Legal Aid NSW hutuma mawakili wa zamu kwa mahakama zote za mitaa na mahakama nyingine nyingi na mabaraza kote NSW. Mawakili wa zamu huwasaidia watu ambao wana kesi mahakamani siku hiyo na ambao hawana wakili wao wenyewe.

Mawakili wa zamu hufanyia kazi kwa Legal Aid NSW au ni mawakili wa kibinafsi wanaolipwa na Legal Aid NSW ili kukusaidia. Unaweza kuangalia ili uone ni wapi wanapatikana katika ukurasa wetu wa tovuti wa Help at NSW courts and tribunals (Msaada kwa mahakama na baraza za NSW).

Ni bora kupata usaidizi wa kisheria kabla ya kwenda mahakamani. Pigia simu kwa timu yetu ya LawAccess NSW kupitia 1300 888 529 au ubofye kitufe cha kuwasiliana nasi ili kuzungumza na timu kwenye gumzo la wavuti.

Husaidia katika mahakama za mitaa ya Bankstown, Blacktown, Penrith, Mount Druitt na Sutherland

Je! una kesi ya jinai katika:

  • Mahakama ya Mtaa ya Bankstown
  • Mahakama ya Mtaa ya Blacktown
  • Mahakama ya Mtaa ya Mt Druitt
  • Mahakama ya Mitaa ya Penrith, au
  • Mahakama ya Mtaa ya Sutherland?

Kuna njia rahisi ya kuomba usaidizi wa kisheria kutoka kwa wakili wa zamu - jaza tu fomu yetu ya mtandaoni. Fomu ni ya haraka, rahisi kutumia na inaweza kuwasilishwa wakati wowote. Baada ya kuwasilishwa, mfanyakazi wa Legal Aid NSW atakupigia simu.

Ikiwa hujui nambari yako ya H, weka H0000 unapoombwa. Fomu hii inaweza kutumika tu kwa mahakama zilizoorodheshwa hapo juu.

Mtu yeyote anaweza kuwasiliana na wakili wa zamu kwa usaidizi mdogo siku ambayo kesi yake iko mahakamani.

Ikiwa kesi yako ni ngumu zaidi, wakili wa zamu anaweza kukusaidia kuomba iahirishwe. Hatua hiyo itaahirisha kesi yako hadi tarehe ya baadaye ili uweze kupata ushauri wa kisheria au uwakilishi. Unaweza kupata habari zaidi katika ukurasa wetu wa wavuti wa Ushauri wa Kisheria.

Kuna mipaka juu ya kile wakili wa zamu anaweza kukufanyia. Wakili wa zamu anaweza kuwa na uwezo wa:

  • kukupa ushauri kuhusu kesi yako
  • kukueleza ni nini kinaweza kutokea mahakamani
  • kukusaidia kuomba ahirisho ili kuahirisha kesi yako hadi tarehe ya baadaye ili upate muda wa kupata ushauri wa kisheria.
  • kuzungumza na mahakama/baraza au wahusika wengine kwa niaba yako
  • kukusaidia kwa hati zako za mahakama au maombi ya dharura ya mahakama, au
  • kuongea kwa niaba yako mahakamani.

Katika masuala ya sheria ya familia, mawakili wa zamu wanaweza pia kukusaidia kwa matatizo ya dharura ya sheria ya familia - kama vile ikiwa mpenzi wako wa zamani hajarejesha mtoto wako au anatishia kumpeleka ng'ambo.

Katika kesi ya jinai hawawezi kukuwakilisha mahakamani ikiwa umekana kosa na kesi yako imeorodheshwa kusikilizwa siku hiyo.

Kikao cha kusikilizwa ni wakati mashahidi wanapofika mahakamani kuzungumzia kilichotokea na hakimu au jaji anazingatia hoja zilizotolewa na mawakili wote wawili.

Iwapo unahitaji usaidizi au unataka mtu aongee kwa niaba yako katika kesi, unapaswa kuzungumza na wakili kutoka Legal Aid NSW au wakili ambaye hutoa msaada wa kisheria vizuri, kabla ya tarehe yako ya kusikilizwa. Unaweza kujua zaidi kuhusu hili katika ukurasa wetu wa tovuti wa Ushauri wa Kisheria.

Tuna mawakili wa zamu katika mahakama zote za mitaa katika NSW, maeneo yote ya family law court (mahakama ya sheria ya familia) wakati mahakama inaketi pale na katika mahakama nyingine nyingi na mabaraza kote NSW.

Unaweza kuangalia kama usaidizi unapatikana katika eneo lako katika ukurasa wetu wa tovuti wa Help at NSW courts and tribunals (Msaada kwa mahakama na baraza za NSW).

Kuona wakili wa zamu na kupokea msaada katika siku ile ni bure.

Ukiendelea kupata usaidizi utahitaji kustahiki usaidizi wa kisheria na utalazimika kulipa mchango kwa gharama ya kesi yako.

Kiasi unachopaswa kulipa kinategemea kiasi unachopata na kile unachomiliki.

Katika masuala ya sheria ya jinai huna haja kustahiki usaidizi wa kisheria ikiwa wakili wa zamu anakupa ushauri tu, au ikiwa ni mwonekano wako wa kwanza na uko kizuizini. Ikiwa wakili wa zamu anakuwakilisha mahakamani kawaida utahitaji kustahiki usaidizi wa kisheria.

Katika masuala ya sheria ya familia huhitaji kustahiki usaidizi wa kisheria ili kupata usaidizi kutoka kwa wakili wa zamu au huduma za usaidizi wa kijamii mahakamani.

Maneno ya kisheria wakati mwingine ni magumu kuelewa. Ikiwa Kiingereza sio lugha yako ya kwanza au unapendelea kuwasiliana katika Auslan (Lugha ya Ishara ya Australia), unaweza kuchagua kuwa na mkalimani wa kukusaidia mahakamani.

Mara nyingi mahakama itamlipa mkalimani, na unapaswa kuwasiliana nayo ili ipange haraka iwezekanavyo.

Ikiwa mahakama itaamua kuwa mkalimani anahitajika, inaweza kuwa muhimu kuahirisha suala hilo hadi tarehe ya baadaye.

Ikiwa unahitaji mkalimani au usaidizi mwingine wa mawasiliano ili kuwasiliana nasi, tafadhali angalia chaguo kwenye ukurasa wetu wa tovuti wa Wasiliana nasi.

Unapokuja mahakamani unapaswa:

  • kukusanya na kuleta nyaraka zote ulizo nazo kuhusu suala lako – katika masuala ya jinai hizi zinaweza kujumuisha karatasi za ukweli za polisi na marejeleo ya wahusika, katika masuala ya sheria ya familia hizi zinaweza kujumuisha nakala za amri zozote na hati nyingine za mahakama, katika masuala ya madai hizi zinaweza kujumuisha nakala za barua au notisi za adhabu zinazohusiana na suala lako la kisheria
  • kufika kwa mahakama saa moja kabla ya kesi yako – unaweza kuhitaji kusubiri kuonana na wakili wa zamu
  • hakikisha una siku nzima – baadhi ya mahakama huorodhesha kesi zote kwa wakati mmoja hivyo unaweza kusubiri saa chache kabla ya mahakama kusikiliza kesi yako, unapaswa kuuliza mahakama
  • ijulishe mahakama ikiwa unahitaji mkalimani au usaidizi mwingine, na
  • uende na rafiki au mtu wa familia kwa usaidizi ikiwa unataka.

Ikiwa una wasiwasi kuhusu usalama wako mahakamani, unapaswa kuwasiliana na mahakama kabla ya tarehe yako ya mahakama ili kujadili matatizo yako, zungumza na walinda usalama unapoingia kwenye jengo la mahakama au utumie maelezo katika ukurasa wetu wa tovuti wa Wasiliana nasi ili kuzungumza nasi kabla ya kwenda mahakamani.

Huenda wakili wa zamu asiweze kumaliza kesi yako siku ile utakapofika mahakamani. Ikiwa kesi yako ni ngumu zaidi, wakili wa zamu anaweza kukusaidia kuomba iahirishwe (kuweka suala lako hadi tarehe ya baadaye) ili upate nafasi ya kupata ushauri wa kisheria au uwakilishi.

Iwapo unahitaji usaidizi zaidi wa kisheria, mawakili wa zamu kutoka Legal Aid NSW wanaweza kuendelea kukusaidia au kukusaidia kutuma maombi ya msaada wa kisheria kwa wakili kuendesha kesi yako. Unaweza kusoma zaidi katika ukurasa wetu wa Tuma Ombi la usaidizi wa kisheria. Tunaweza pia kukuelekeza kwa huduma zingine ambazo zinaweza kukusaidia.

Watu wa asili na Torres Strait Islander wanaweza kupata usaidizi mahakamani kutoka kwa mawakili wa zamu wa Legal Aid NSW au mawakili kutoka Aboriginal Legal Service (NSW/ACT) (Huduma ya Kisheria ya Asili (Aboriginal)).

Iwapo una umri wa chini ya miaka 18 na unahitaji usaidizi mahakamani, piga simu kwa nambari ya Dharura ya Vijana kupitia 1800 10 18 10.

Simu ya dharura hufanya kazi saa tatu asubuhi hadi saa sita za usiku katika siku za wiki, na ina huduma ya saa 24 kutoka Ijumaa, saa tatu asubuhi hadi Jumapili saa sita za usiku na pia katika likizo za umma.

Women's Domestic Violence Court Advocacy Services (Huduma za Utetesi za Wanawake za Mahakama ya Mateso ya Nyumbani) husaidia wanawake na watoto wanaopitia unyanyasaji wa nyumbani katika mahakama nyingi za mitaa karibu na NSW.

Wafanyakazi wa usaidizi kwa wanawake na wanaume kutoka Family Advocacy and Support Services (Huduma za Utetesi na Usaidizi wa Familia) wanapatikana ili kusaidia familia zilizoathiriwa na unyanyasaji wa nyumbani katika mahakama za sheria za familia.

Wafanyakazi wa Vijana kutoka Mpango wa Msaada wa Mahakama ya Watoto huwasaidia vijana wanaofika katika Mahakama ya Watoto.